Monday, October 24, 2022

MABADILIKO YA TABIA NCHI

            [Picha kwa Ihsani ya Pinterest]

Nini maana halisi ya Mabadiliko ya tabia nchi? Ni madiliko yanayo sababishwa na kubadilika kwa hali ya hewa inayokaa kwa mda mrefu ambayo inaleta athari duniani.Watu wingi hudhani Ukame pekee ndio huletwa na mabadiliko ya tabia nchi ila sivyo,hali yeyote ya hewa inapokaa kwa mda mrefu na kuleta athari kubwa hayo ni mabadiliko ya tabia nchi.Hatuwezi kuzungumzia mabadiliko ya tabia nchi bila kuzungumzia kiwango cha joto kinachozidi kila uchao kwa sababu kuongezeka au kupungua kwa joto ndio huleta mabadiliko ya tabia nchi Ulimwenguni.                                                                                

                    
[Picha kwa Ihsani ya Google.]

Tangu mwaka 1950 mapinduzi ya viwanda yalipotokea Joto katika uso wa dunia limeongezeka kwa nyuzi joto 0.8 na hiyo imesababishwa hasa na shughuli za kibinadamu ambazo zimeongeza kiwango cha gesi joto[global warming]katika anga,kuongezeka huko kumepelekea tabaka la Ozoni lenye kazi ya kudhibiti kiwango cha joto kinacho ingia na kutoka kwenye Uso wa dunia kuharibika na kushindwa kudhibiti kiwango cha joto kinacho ingia na kutoka.Ongezeko hilo linaweza kuonekana dogo Sana kwa akili ya kawaida ya binadamu lakini lina athari kubwa sana kwenye uso wa dunia.


Kumekuwa na harakati mbalimbali zinazo fanyika ili kupunguza kiwango cha joto ulimwenguni zikiwemo Harakati za kutoa elimu kwa Raia kuhusu athari za mabadiliko ya hali ya hewa na jinsi ya kukabiliana na janga hilo.Pili, kuna harakati za nchi kupunguza uzalishaji wa gesi joto kwenye viwanda vyao ambavyo ndio chanzo namba moja cha uharibifu wa hali ya hewa.Pia kumekuwa na jitihada mbalimbali za wananchi  kulazimisha serikali zao kuchukua hatua muafaka za kukabiliana na janga hili kupitia midahalo na maandamano.


Wakati wanasayansi wanasema  kuongeza kwa Nyuzi joto 2 kutaiweka dunia katika hali ya hatari,ripoti ya mwaka 2013 ya IPCC inaonyesha kuwa kiwango cha joto kitaongezeka hadi nyuzi 1.5 kufikia mwishoni mwa karne ya 21 kama hakuta chukuliwa hatua  zozote,Aidha ripoti hio imesema mabadiliko ya tabia nchi yanaweza kukabiliwa endapo tu dunia kwa ujumla itafanya mabadiliko kwenye maeneo mengi.


                  [Picha kwa Ihsani ya Google]

Athari ambazo zitaendela kuikumba dunia endapo hatutachukua hatua mwafaka ni kupanda kwa Kiwango cha maji baharini ambapo itapelekea baadhi ya Visiwa kufurika na vengine kuzama kabisa.Shirika la  Afya Duniani "WHO" limeonya kuwa mabadiliko hayo yatapelekea kuongezeka kwa magonjwa kama Nimonia na Utapiamlo ambao unasababishwa na ukosefu wa lishe bora ambao utakuwa ni tatizo kubwa kwa nchi za Afrika.Makadirio ya WHO yanaonyesha watu 140,000 hupoteza maisha kila mwaka kwa sababu ya mabadiliko ya tabia nchi.

Ni jukumu letu sote  kukabiliana na janga hili na kuhakisha lina tokomea.

                                                             By Dago Rajaab.


22 comments:

  1. Kweli kabisa ...dunia kwa ujumla yawezafanya mabadiliko kwenye maeneo mengi ili ikipuuza magonjwa yataibuka 😥

    ReplyDelete
  2. Kazi safi sana kaka
    Serikali nayo inafaa kuwajibika mara dufu ili kuangamiza janaga hili.

    ReplyDelete

Maisha ya Chuoni

                  Picha kwa hisani ya Dago Muller Maisha ya chuo kikuu yanasemekana kuwa ya kufurahiwa na ya kukumbukwa katika maisha ya kil...