Monday, October 17, 2022

FAHARI YA PWANI

                 Picha Kwa Hisani ya Google

Tangu jadi halmashauri ya Bandari ya Mombasa imekuwa Fahari ya wakaazi wa mvita na pwani kwa ujumla kwa sababu imekuwa ikitoa fursa nyingi zikiwemo kuajiri maelfu ya wakaazi wa pwani na imekuwa ikitoa Fursa ya kuendesha shughuli za Uchukuzi zikiwemo biashara ya Usafirishaji wamizigo ambazo pia kivyake zimeajiri mamia ya watu ambao wanategemea bandari ili kuendesha maisha yao ya kila Uchao.

                 Picha Kwa Hisani ya Google

Mnamo Disemba mwaka 2019 fahari hii iliingia doa pindi tu Rais Mstaafu Uhuru kenyatta alipo agiza shughuli za Halmashauri ya bandari ya Mombasa kuhamishwa kwenye kaunti ndogo ya Naivasha,Habari hii ili watamausha wa Pwani na wapo wachache walio simama kidete kupinga udhalili huo,akiwemo aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Mvita Mheshimiwa Abduswamad ambapo hakufanikiwa kuupinga uamuzi huo.

Kitendo hiki kilipelekea maelfu ya  watu kupoteza ajira na kuzidi kuzorotesha uchumi wa wananchi wa pwani ambao walizalimika kuukumbatia Umaskini na Umaskini ukawa vazi Lao.

Ni miezi kadhaa sasa imepita tangu tumeingia debeni na kupiga kura kilio chetu kikubwa kilikuwa kurudishwa kwa shughuli zote za Halmashauri ya bandari ndani ya Pwani iliziweze kuwafaidisha wazawa,Rais William Ruto aliinuka kidedea na kuamrisha mara moja shughuli zote kurejeshwa rasmi kwenye bandari ya mombasa.

Wakaazi walipongeza kwa hatua hii kwa sababu Ukiritimba wa S.G.R juu ya uchukuzi wa Mizigo umeharibu uchumi wa bandari ya Mombasa katika kipindi cha miaka mitatu ambapo maelfu ya wamiliki wa lori na madereva walipoteza maisha yao ambapo vituo vya kigeni vya kontena vilikosa manufaa na maelfu ya watu wanaofanya kazi katika uuzaji wa malori, vituo vya huduma ya mafuta, mitambo, wafanyabiashara wa vipuri waliachwa bila kazi.


                  Picha Kwa Hisani ya Google

Kongole kwa Amiri Jeshi Mkuu na Rais William Ruto kwa kuondosha udhalimu huu na tuendelee kumuombea kwa Maulana azidi kuendelea kutatua madhila ya pwani.

                                                       By Dago Rajaab.

28 comments:

  1. Nawe pia kongole kwa kazi njema ulioifanya
    Hongera kaka

    ReplyDelete
  2. Waah lugha uliyotumia mufti kabisa 😊

    ReplyDelete
  3. This Mombasa and Mombasa is our Business

    ReplyDelete

Maisha ya Chuoni

                  Picha kwa hisani ya Dago Muller Maisha ya chuo kikuu yanasemekana kuwa ya kufurahiwa na ya kukumbukwa katika maisha ya kil...